1 Corinthians 12:1-3

Karama Za Rohoni

1 aBasi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu. 2 bMnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena. 3 cKwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.

Copyright information for SwhNEN